Wanandoa  wawili  Adam Charles Mtambo  
41 na  Mkewe  Catalina  Gabriel  39  wakazi  wa  Kitongoji cha Kasekese 
 B  Kata ya  Kasekese  Wilaya ya   Tanganyika   Mkoa wa  Katavi   
wameuawa  kikatili kwa  kukatwa na  mapanga na  kushambuliwa kwa silaha 
za jadi katika  sehemu mbalimbali za  mwili wao wakati wakiwa wamelala 
pamoja   kwenye kitandani kwao.Mwandishi wa Malunde1 blog,Walter Mguluchuma anaripoti.
Afisa  Mtendaji wa   Kata  hiyo ya  Kasekese  Ramadhani  Ibrahim alisema
    kuwa tukio hilo la  mauaji  hayo ya kikatili limetokea  usiku wa 
kuamkia  leo Jumamosi Oktoba 14,2017  majira ya saa saba kasorobo 
nyumbani kwa  wanandoa  hao .
Alisema   marehemu   Adam ambae  alikuwa ni  mfanya  biashara  
anayemiliki maduka  mawili  Kijijini   hapo, siku  hiyo   alifanya   
biashara ya kuuza  duka  kama  ilivyo  kawaida  yake na  baada ya muda 
wa  kufunga duka  ulipofika   alifunga na waliingia ndani  nyumba yao 
kulala  yeye na  mke wake.
Alieleza kuwa wakati wakiwa  wamelala  ndani walitokea wauaji hao   
ambao  wanasadikiwa kuwa watatu na walifyatua risasi tatu za  bunduki 
hewani na kisha walivunja  mlango  na kuingia  ndani ya chumba  moja kwa
 moja walichokuwa wamelala    wanandoa hao.
Alisema baada ya kuingia  chumbani waliwakuta  wanandoa hao wamelala 
kitandani na  ndipo walipoanza kuwashambulia kwa kuwakata kata kwa   
panga katika sehemu za usoni na kichwani na  kuwashambulia  kwa kutumia 
silaha za  jadi  ikiwemo marungu na fimbo.
Asifa  Mtendaji  huyo wa kata  alieleza  kuwa  marehemu   alijaribu 
kuwasihi waache kuwashambulia na   aliwaeleza  kuwa  kama  shida yao ni 
 fedha  basi  waache kuwakata kwa mapanga na kuwashambulia kwa silaha za
  jadi  na yeye  yuko  tayari kuwaonyesha  mahali  fedha  zake  zilipo 
ili wasiendelee  kuwashambulia.
Pamoja  na  kuwasihi hivyo wauaji hao waliendelea kuwashambulia tu kwa  
mapanga  hali  ambayo iliwafanya  marehemu na  mkewe wazidi kupiga  
mayowe ya kuomba msaada kwa  majirani wao .
Alisema  kutokana na  mayowe  hayo  watoto wa  marehemu ambao  nao 
walikuwa wakiishi kwenye  nyumba  hiyo wakiongozwa na  kaka yao  aitwaye
   Charles waliingia  chumbani kwa  wazazi wao kwa lengo la kutoa 
msaada.
Hata  hivyo walishindwa kutoa  msaada baada ya  kushambuliwa na watu hao
 kwa kuwapiga na marungu na fimbo hali ambayo iliwafanya wakimbilie  
kwenye vyumba vyao vya kulala na kujifungia .
Majirani walifika  kwenye  eneo hilo na  walikuta  mlango wa  mbele wa  
nyumba hiyo ukiwa umevunjwa na walipoingia  kwenye chumba walichokuwa 
wanalala marehemu hao waliwakuta wakiwa wamelala  chini ya kitanda huku 
wakiwa   na majeraha makubwa katika sehemu mbalimbali za mwili wao huku 
damu  zikiwa zimetapakaa  kwenye chumba hicho .
Mwenyekiti wa  Kitongoji cha   Kasekese  Happnes  Bona  alisema jitihada
 za kutafuta usafiri kwa  ajili ya kuwafirisha wanandoa  hao kwa  ajili 
ya kuwapeleka katika  Hospitali ya   Wilaya ya  Mpanda zilifanyika na  
hata hivyo wakati wakiwa njiani  baada ya muda mfupi   wanandoa hao 
walifariki.
Alisema  tangu amekuwa  Mwenyekiti wa  Kitongoji  hicho hajawahi kuona  
mauaji ya kutisha na y akikatili  kiasi hicho kwani marehemu  hao 
waliuawa kwa kukatwa  katwa  kama   wanyama na sio kama  binadamu .
Kwa  mujibu wa  Mwenyekiti  huyo   miili ya  marehemu hao imehifadhiwa  
katika  chumba  cha kuhifadhi maiti  katika  hospitali ya  Wilaya ya  
Mpanda na  baada ya uchunguzi wa kidaktari.
Katika hali inayotajwa kuwa huenda vifo hivyo vimetokana na visasi,wauaji hao hawakuondoka na kitu chochote baada ya kutekeleza mauaji hayo.
Jeshi la polisi mkoani Katavi limethibitisha kutokea kwa tukio hilo.

 
 
 Posts
Posts
 
 
 
 
 
0 comments: