JITIHADA ZA KUMPELEK TUNDU LISSU ZAGONGA MWAMBA
Mbunge
 wa Singida Kaskazini Lazaro Nyalandu ambaye amekuwa akifuatilia kwa 
ukaribu matibabu ya mbunge mwenzake wa Singida Mashariki Tundu Lissu, 
ameweka wazi kwamba jitihada za kumpeleka Lissu Marekani kutibiwa kwa 
sasa zimegonga mwamba.
Lazaro
 Nyalandu ametoa taarifa hiyo kwenye ukurasa wake wa facebook ambapo 
amendika ujumbe kuhusu kauli ya madaktari wanaomtibu Tundu Lissu jijini 
Nairobi Kenya, na kueleza kwamba madaktari hao wamesema hawawezi 
kuruhusu Tundu Lissu asafirishwe kupelekwa Marekani kutokana na hali 
yake jinsi ilivyo.
“Kwa
 sasa mipango ya kumsafirisha Mheshimiwa Tundu Lissu nje itasimama 
kutokana na ushauri wa madaktari wa hospitali ya Nairobi, ili kuruhusu 
kukamilishiwa huduma za tiba ambazo tayari ameanzishiwa hadi hapo 
itakavyoshauriwa au vinginevyo, ama endapo kutatokea umuhimu wa kufanya 
hivyo katika siku zijazo”, ameandika Lazaro Nyalandu.
Hapo
 jana Lazaro Nyalandu alitoa taarifa kwamba wanafanya jitihada za 
kumpeleka Tundu Lissu Marekani kwa ajili ya matibabu zaidi, huku 
wakisubiria ripoti ya madaktari wa hospitali ya Nairobi ambako mbunge 
huyo anatibiwa, na ndipo ilipokuja taarifa hiyo kwamba haitowezekana 
kumsafirisha kwa sasa.
Ikumbukwe 
 kuwa Mbunge Tundu Lissu alipigwa risasi na watu wasiojulikana Septemba 
7, 2017 mjini Dodoma majira ya mchana, na usiku wa siku hiyo hiyo 
alikimbizwa jijini Nairobi kwa ajili ya matibabu zaidi, kutokana na hali
 yake kutokuwa nzuri.
==>>Huu ni ujumbe alioundika Lazaro Nyalandu
TUNAFAHAMU
 kwamba, tangu Alhamisi, Septemba 7, siku ambayo Mh #TunduLissu, Mb., 
(Singida Mashariki-CHADEMA) alishambuliwa kwa kupigwa risasi mjini 
DODOMA, Watanzania wengi wamesononeshwa na kulia sana, na kubwa zaidi, 
WOTE wameungana katika kuomba Sala na Dua kwa ajili ya Mh #TunduLissu, 
ili mkono wa Mkombozi, aliye MUNGU wetu, upate kumgusa tena na kumponya 
dhidi ya majeraha, maumivu na mateso anayoyapitia.
MAPEMA leo, baada ya kutembelea #NairobiHospital asubuhi, nimefanya 
mazungumzo mchana wa leo na Mh #FreemanMbowe, ambapo kwa pamoja 
tumeelezwa kuwa MADAKTARI #NairobiHospital wameendelea na kumtibu Mh 
#TunduLissu, ikiwa ni pamoja na kuanza upasuaji, na huduma zingine za 
Kitabibu walizomwanzishia tangu awasili Nairobi siku ya Alhamisi, 
Septemba 7. IMEELEZWA vilevile kuwa kwa sasa Mh #TunduLissu ataendelea 
na TIBA hospitalini hapo kutokana na kile kilichoelezwa kuwa hali yake 
bado ni "Critical but stable", na KWAMBA mwili wake unaendelea kuitikia 
vema matibabu lukuki anayofanyiwa kwa wakati mmoja.
KWA SASA, mipango ya kumsafirisha Mh #TunduLissu NJE itasimama, kutokana
 na ushauri wa MADAKTARI #NairobiHospital, ili kuruhusu kukamilishiwa 
huduma za TIBA ambazo tayari ameanzishiwa, hadi hapo itakavyoshauriwa 
vinginevyo, ama endapo kutatokea umuhimu wa kufanya hivyo katika SIKU 
zijazo.
AIDHA, SOTE tuzidi KUMWOMBEA MUNGU na kushiriki katika CHANGIZO za kusaidia gharama za matibabu yake.
NI DHAHIRI kwamba Wana Singida, na Watanzania WOTE tumeumia, tumekwazwa,
 na tumesononeshwa sana kwa uonevu na dhuluma aliyotendewa ndugu yetu Mh
 #TunduLissu. Kitendo hiki hakikubaliki mbele za MUNGU na mbele za 
wanadamu.
Tunaiomba Serikali yetu iendeleze juhudi zake na kuchukua hatua za 
haraka kuwasaka, kuwakamata, na kuwatia mbaroni watu wote waliohusika 
kupanga na kutekeleza shambulio hili la kigaidi dhidi ya Mh #TunduLissu.
 Aidha, shambulio hilo walilolifanya watu wasiojulikana limedhalilisha 
taifa, na kudhoofisha taswira ya kukomaa kwa demokrasia inayoruhusu 
kuvumiliana na kuheshimiana licha ya tofauti zetu za kiitikadi na 
mitazamo ya kisiasa.
HALIKADHALIKA, kwetu sote kama TAIFA, huu ni wakati wa Watanzania wote 
kuwa wamoja, bila kujali tofauti zetu za kiitikadi, kidini, wala 
kikabila, tuungane na kulaani kitendo hiki na vitendo vyote vya uonevu 
na kuumizana. TANGU zamani, IMEANDIKWA: Haki HUINUA Taifa.
Lazaro S Nyalandu, Mb.
Singida Kaskazini-CCM
Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM (TAIFA)


 
 
 Posts
Posts
 
 
 
 
 
0 comments: