JOSEPH YONA HAIKUBALIKI KUWAKUMBATIA WABADHIRIFU


Mwenyekiti wa chama cha mapinduzi tawi la bokorani Mh Joseph Yona amesema naunga mkono jitihada za Rais na Mwenyekiti wa ccm Taifa Mh John Magufuli katika kulinda na kusimamia mali za Nchi na chama

Alisema ilifika sehemu nchi hii ikawa pango la walanguzi kila mtu anafanya kivyake sasa basi ubadhilifu ndani ya nchi hii marufuku tunataka Taifa lenye kuendeshwa katika misingi na sheria tulizo jiwekea 

Joseph Yona alisema kila mtu awajibike katika nafasi yake mimi nitawajibika katika tawi langu na kila mmoja awajibike katika nafasi yake 

Mh Yona alisema kuwa sita mfumbia macho yeyeto atakae shindwa kuzilinda mali za chama katika mazingira yangu hata awena nafasi kiasi gani

Mh Joseph Yona aliyasema hayo leo katika kikao cha mkutano mkuu wa kata ya mtoni kilichofanyika katika ukumbi wa ccm mtoni

Mh Yona Akichangia mada mbele ya wajumbe wa mkutano mkuu wa kata ya mtoni 

Wajumbe wa mkutano mkuu wa kata ya mtoni wakisikiliza hoja ya Mh joseph Yona

0 comments:

Mh MPUTA AMESEMA MAGUFULI KATUFANYA TUTEMBEE KIFUA MBELE

Mwenyekiti wa chama cha mapinduzi ccm kata ya mtoni Mh Mputa Zeno Maokola  amejikuta kushindwa kujizuia hisia zake juu ya Rais na Mwenyekiti wa ccm Taifa Dr Magufuli

 Mh MPUTA amesema saivi Magufuli kutufanya tutembee kufua wazi na jezi zetu za chama mtaani bila woga kwani yanayotendeka na Mwenyekiti wa Chama ni makubwa na niyakujivunia aidha Mwenyekiti huyo alisema kwa juhudi zake yeye na uongozi wake hayo kubali kuipoteza kata tena mikononi mwa wapinzani na kuahidi kushughulikia aina yoyote ya makundi ndani ya chama sisi sote kundi letu ni ccm

Mh Mputa amepinga vikali matumizi mabovu ya madaraka kwa viongozi wa chama kuanzia Ngazi yake mpaka katika Mashina tuwahudumie wananchi maana ndio waajiri wetu tufanye kazi katika mazingira ya kuheshimu haki na misingi ya utawala bora

Mh Mputa aliyasema hayo leo katika kikao nawajumbe wa mkutano mkuu kata ikiwa ni mkimbisho wa watendaji wote dani ya kata kutoka katika matawi yote na mashina ndani ya Mtoni
Pichani ni wajumbe wa mkutano mkuu wa kata wakisikiliza yale yaliyo pagwa kufanywa na uongozi waMh Mputa
Mwenyekiti wa chama cha mapinduzi tawi la bokorani Joseph Yona alichangia msaada katika kikao

0 comments:

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumatano ya January 3


0 comments:

Spika Ndugai Amjibu Tundu Lissu


Spika  wa Bunge Job Ndugai amefunguka na kusema Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu pamoja na familia yake hawatambui kuwa Serikali hasa Bunge limeanza kufanya mazungumzo na watu wanaotaka kumsafirisha kwenda nje kwa matibabu zaidi.

Ndugai amedai anatambua kuwa Tundu Lissu atasafirishwa na kwenda kwa matibabu zaidi nje ya Kenya ingawa hajajua ni lini lakini amesema kuwa watu ambao wamepanga kumpeleka huko kwenye matibabu tayari walishamtafuta yeye na kusema watashirikiana nao katika masuala ya matibabu.

"Ni kweli kwamba atapelekwa nje zaidi ya Nairobi ila bado sijui mpaka sasa ni lini kwa kuwa sijajua tarehe bado japo nadhani itakuwa hivi karibuni na wale wanaomgharamia kumpeleka nje wameshawasiliana na mimi na hakika familia ya Lissu hata Tundu Lissu mwenyewe hajui hilo, anafikiri ni wao peke yao lakini najua na walishafika kwangu na kusema watagharamia wao" alisema Ndugai

Spika Ndugai alizidi kueleza kuwa endapo watakubaliana na watu hao basi wao kama Serikali watagharamia katika mambo mengine ambayo yatawashinda hao wadau ambao walimfuata na kuongea naye.

"Gharama ambazo sisi tunaweza kuziingia endapo tutakubaliana na maamuzi hayo kufanyika itakuwa katika yale mambo mengine yanayobakia ambao wale kama wadau, wawezeshaji, wanaotusaidia hawataweza kutoa na ili liafikiwe lazima tuwe na uhakika kitu gani kinalipiwa na kitu gani hakilipiwi vinginevyo tutalipa mara mbili mbili sisi tunalipa wenzetu wanalipa ambapo kidogo italeta mchanganyiko usiokua na afya" alisisitiza Ndugai

Mwaka jana Tundu Lissu alidai kuwa Serikali pamoja na Bunge bado walikuwa hajachangia jambo lolote katika matibabu yake ambayo yanaendelea mpaka sasa nchini Kenya jijini Nairobi kufuatia shambulio lake la kupigwa risasi Septemba 7, 2017 akiwa mjini Dodoma.

0 comments:

Umoja wa mataifa washusha Rungu kwa rais wa congo (DRC)




Umoja wa Mataifa umemwambia Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) Joseph Kabila kutimiza ahadi aliyoiweka ya kuachia madaraka na kupisha uongozi mwingine kuiongoza nchi hiyo hususani wakati huu ambapo nchi hiyo imejaa migomo na maandamano ya kushinikiza ajiuzulu.

Rais Kabila mwenye miaka 46, ameiongoza DRC kwa miaka 17 na msimu wake wa mwisho wa uongozi uliisha tangu December 31, 2016 na akatakiwa aachie ngazi lakini uchaguzi wa kupata Rais na viongoi wapya umekuwa ukiahirishwa mara kwa mara.

Suala hili limesababisha vurugu na maandamano ya raia wa DRC ambao hata hivyo inaelezwa kuwa wamekuwa wakipigwa na askari polisi jamabo ambalo kwenye taarifa ya Umoja wa Mataifa iliyotolewa December 31, 2017 imelaani vikali vitendo hivyo hususani Jijini Kinshasa ambapo watu watano waliuawa na polisi siku hiyo vya Jumapili kwenye maandamano.

0 comments:

TRA Wakomaa na Askofu Kakobe.....Wadai Hawana muda wa Kubishana nae Zaidi ya Kuchunguza Utajiri wake



Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), imemuibukia kivingine, Askofu wa Kanisa la Full Gosper Bible Fellowship (FGBF), Zakaria Kakobe, kuhusu utajiri alionao ikisema haina muda wa kulumbana naye, bali inatekeleza maelekezo ya Kamishna Mkuu.

Aidha, mamlaka hiyo imesema haitaki kuwa kwenye malumbano na askofu huyo wakati ikiendelea na uchunguzi dhidi ya vitega uchumi vyake na kuangalia kama analipa kodi ya serikali.

Mkurugenzi wa Elimu kwa Mlipakodi wa TRA, Richard Kayombo, jana alisema maofisa wao wanaendelea kutekeleza tamko la Kamishna Mkuu wa TRA, Charles Kichere, la kuchunguza utajiri wa Askofu Kakobe.

"Sisi (TRA) hatutaki kuwa kwenye malumbano na Kakoke, tulichosema tumeishia hapo. Alichosema Kamishna Mkuu tunaishia hapohapo, hatutakiwi kujibishana naye," Kayombo alisema.

Katika mkutano wake na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam Jumamosi, Kichere alisema mamlaka yake imeipokea kwa furaha kauli ya Askofu Kakobe kuhusu utajiri wake na inataka kujiridhisha vyanzo vya utajiri huo.

Kichere alisema TRA inafahamu kuwa shughuli za kidini hazitozwi kodi, lakini inataka kufahamu kama fedha hizo za Askofu Kakobe zinatokana na sadaka pekee.

Alisema wameamua kuchukua uamuzi huo kutokana na kiongozi huyo wa kiroho kutokuwamo katika kumbukumbu za ulipaji kodi za TRA.

Kauli iliyoleta utata na kuibua uchunguzi huo ni ya Askofu Kakobe kukaririwa wiki iliyopita akidai ana fedha nyingi kuliko serikali na anao uwezo wa kumkopesha waziri pindi akiombwa kufanya hivyo.

Hata hivyo, juzi ikiwa ni siku moja baada ya TRA kutangaza kufanya uchunguzi dhidi yake, Askofu Kakobe alieleza historia ya maisha yake, mali za kanisa na zake na misukosuko aliyopitia na kusisitiza kuwa tafsiri iliyofanyika dhidi ya kauli yake kuhusu utajiri ni ya kimwili na siyo ya kiroho. Alidai kauli yake ilimaanisha yeye ni tajiri wa kiroho na si fedha.

Askofu Kakobe aliishauri TRA kutohangaika naye, badala yake ikatafute fedha mahali kwingine akieleza kuwa ana nyumba moja iliyopo Kijitonyama jijini na aliijenga mwaka 1986 kwa gharama ya Sh. milioni mbili ikiwa ni pamoja na gharama za kiwanja.

Huku akishangiliwa na waumini wa kanisa lake kwenye ibada ya kuuaga mwaka 2017, Askofu Kakobe pia alidai kuwa mwaka 1995 alinunua gari aina ya Nissan Patrol kwa kutumia sadaka za washirika wa kanisa na hivi karibuni waliibuka watu waliochangishana na kumnunulia gari jingine.

Alidai kuwa hata kwao Kakonko, Kigoma hajawahi kujenga hata choo na kilichopo ni makaburi ya wazazi wake waliozikwa kwenye eneo la kuingia kwenye nyumba iliyojengwa na wazazi wao.

Askofu Kakobe pia alidai kuwa kanisa la FGBF ndani na nje ya nchi halina mradi wowote wa kiuchumi kama shamba au hoteli na akasisitiza serikali ichunguze kote huko.

Alibainisha kuwa makusanyo yote ya sadaka huhifadhiwa kwenye akaunti iliyofunguliwa mwaka 1990 katika Benki ya NBC na ni mali ya bodi ya wadhamini ambayo imesajiliwa Wakala wa Usajili, Ufilisi na Udhamini (Rita).

0 comments:

Breaking News: Televisheni 5 Nchini Zapigwa Faini na TCRA kwa Kukiuka Maadili ya Utangazaji


Mamlaka ya mawasiliano Tanzania, TCRA, imevipiga faini vituo vitano vya Televisheni  kwa makosa ya ukiukwaji wa taratibu za kutangaza taarifa ya habari hapa nchini.

Adhabu hiyo imetangazwa leo na Makamu mwenyekiti wa kamati  ya Maudhui ya Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) , Joseph Mapunda

Kituo cha runinga cha EATV, kimetozwa faini ya jumla ya TZS milioni 15, kwa makosa matatu ikiwemo, kukiuka maadili ya uandishi na kutangaza habari za uchochezi. Faini hiyo inapaswa kulipwa ndani ya siku 30, na kituo hicho kitawekwa chini ya uangalizi kwa muda wa miezi 6.

Aidha, TCRA imekitoza faini ya TZS milioni 15 kituo cha Runinga cha Channel ten, kwa makosa ya kutangaza habari ambazo hazikuzingatia maadili ya uandishi, kutangaza habari za uchochezi, na kutozingatia mizania. Pia kituo hicho kitawekwa chini ya uangalizi kwa miezi sita kuanzia leo.

Kituo cha runinga cha Star TV, kimetozwa faini ya jumla ya TZS milioni 7.5 kwa makosa matatu ikiwemo, kukiuka maadili ya uandishi na kutangaza habari za uchochezi. Faini hiyo inapaswa kulipwa ndani ya siku 30 na pia kituo hicho kinawekwa chini ya uangalizi wa miezi 6.

Pia TCRA imekitoza faini ya TZS milioni 7.5 kituo cha runinga cha Azam Two, kwa makosa ya kutangaza habari za uchochezi, kutangaza habari ambazo hazikuzingatia maadili ya uandishi na kutozingatia mizania. Pia kituo hicho kitawekwa chini ya uangalizi kwa miezi sita kuanzia leo. 

Kituo cha runinga cha ITV, kimetozwa faini ya jumla ya TZS milioni 15, kwa makosa matatu ikiwemo, kukiuka maadili ya uandishi na kutangaza habari za uchochezi. Faini hiyo inapaswa kulipwa ndani ya siku 30, na kituo hicho kitawekwa chini ya uangalizi kwa muda wa miezi 6.

0 comments:

Breaking News: Babu Seya na Mwanaye Watinga Ikulu Kumshukuru Rais Magufuli kwa Kuwasamehe


Mwanamuziki Nguza Vicking “Babu Seya” na wanae Johnson Nguza “Papii Kocha”, Francis Nguza na Michael Nguza walipofika Ikulu jijini Dar Leo Januari 2, 2018 kumshukuru Rais Magufuli kwa msamaha wake aliotoa kwao dhidi ya kifungo cha maisha walichokuwa wakitumikia
Rais Dkt John Pombe Magufuli akiwa ameshikana Mikono na kuomba dua na Mwanamuziki Nguza Vicking “Babu Seya” na wanae Johnson Nguza “Papii Kocha”, Francis Nguza na Michael Nguza walipofika Ikulu jijini Dar Leo Januari 2, 2018 kumshukuru kwa msamaha wake aliotoa kwao dhidi ya kifungo cha maisha walichokuwa wakitumikia

2 comments:

Waziri Mkuu: Vijana Jitokezeni Mlime Korosho


WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amewataka vijana wanaioishi kwenye mikoa ambayo zao la korosho linastawi wachangamkie kilimo cha zao hilo kwa sababu lina fursa nyingi.

“Mahitaji ya korosho ni makubwa duniani, korosho zinatumika mahotelini na kwenye mikutano mikubwa, zinatumika kwenye ndege, kwa hiyo bei yake lazima iwe kubwa,” alisema.

Ametoa wito huo Jumapili, Desemba 31, 2017 wakati akizindua kampeni ya kitaifa ya upandaji mikorosho bora na mipya milioni 10 msimu wa 2017/2018 mjini Ruangwa, mkoani Lindi. Kaulimbiu ya kampeni hiyo ni: “Korosho ni dhahabu ya kijani, tuitunze, itutunze”.

Waziri Mkuu alisema anaamini kuwa kijana yoyote mwenye nguvu ya kufanya kazi hawezi kushindwa kulima zao hilo kwa sababu halihitaji uangalizi mkubwa. “Kijana yeyote anaweza kulima zao hili kwa sababu ekari moja ina miche 37 hadi 40. Kuna mtu atashindwa kuangalia miche 37 hadi ikue?” aliuliza.

Waziri Mkuu alisema kilimo cha korosho ni rahisi lakini pia kilimo cha korosho ni rafiki wa mazingira, kwani miti ikikua inatunza mazingira na inasaidia kuleta mvua. Alisema mbali ya mikoa inayolima korosho ya Lindi, Mtwara, Ruvuma Pwani na Tanga, kuna mikoa mingine ambayo udongo wake umepimwa na kubainika kuwa zao hilo linaweza kustawi bila shida.

Aliitaja mikoa hiyo kuwa ni Dodoma, Kigoma, Njombe, Songwe na kuongeza kuwa mikoa ya Singida na Manyara iko mbioni kukamilisha uchunguzi wake.

“Leo tumeanza usambazaji wa miche ya bure hapa Ruangwa ambao najua utafuatiwa na wilaya nyingine hapa nchini. Nimeelezwa kwamba mche wenye kutoa mazao mengi ni wa kuanzia miaka mitatu hadi saba, kwa umri huu miche ya korosho inaweza kuchanganywa na mazao mengine kama ambavyo mtashauriwa na maafisa kilimo ili wakati wa palizi ya hayo mazao, shamba lako la korosho libakie kuwa safi,” alisema.

Waziri Mkuu ambaye pia ni Mbunge wa Ruangwa, yuko kwenye mapumziko ya mwisho wa mwaka jimboni kwake.

Mapema, akitoa taarifa ya taarifa ya uzalishaji wa miche ya mikorosho msimu wa 2017/18 mkoani Lindi, Katibu Tawala wa mkoa huo, Bw. Ramadhani Kaswa alimweleza Waziri Mkuu kwamba katika msimu wa 2016/2017, mkoa huo uliweka lengo la kuzalisha na kupanda miche 1,000,000 ya mikorosho.

“Hadi mwisho wa msimu huu, jumla miche 716,532 ilizalishwa na kusambazwa kwa wakulima sawa na asilimia 71.6 ya lengo lililowekwa. Kati ya hiyo, Halmashauri ya Kilwa ilizalisha miche 55,000, Halmashauri ya Lindi miche 100,000, Manispaa ya Lindi miche 50,000; Halmashauri ya Liwale miche 106,000; Halmashauri ya Nachingwea miche 227,670 na halmashauri ya Ruangwa miche 177,862,” alisema.

“Miche hii iligawanywa kwa wakulima bure ambao walipanda kwenye mashamba yao. Zoezi la tathmini ya miche iliyokua baada ya kupandwa linaendelea kwenye halmashauri zote za mkoa,” aliongeza.

Bw. Kaswa alisema kutofikiwa kwa lengo hilo kumechangiwa na kutopatikana kwa mahitaji yote ya mbegu na vifaa vya uzalishaji, kuchelewa kwa vifaa, na mwamko mdogo wa vikundi vya uzalishaji.

Alisema kwa msimu huu wa 2017/2018, mkoa uliweka lengo la kuzalisha miche ya mikorosho iliyobebeshwa na isiyobebeshwa 7,132,000. Kati ya hiyo, Wilaya ya Kilwa walilenga miche 1,122,000, Lindi Vijijini 1,550,000, manispaa ya Lindi 1,000,000, Liwale miche 450,000, Nachingwea miche 1,810,000 na Ruangwa miche 1,200,000.

“Hadi kufikia tarehe 29 Desemba, 2017 tayari miche 4,974,425 ilikuwa imezalishwa na iko tayari kwa kupandwa kwenye mamlaka za serikali za mitaa kama ifuatavyo:- Kilwa miche 772,000, Lindi Vijijini 1,160,455, manispaa ya Lindi 771,440, Liwale miche 266,000, Nachingwea 991,070 na halmashuri ya Ruangwa imezalisha miche 1,013,460,” alisema.

Sherehe hizo za uzinduzi wa upandaji miche mipya zilihudhuriwa na wakuu wa mikoa ya Lindi, Mtwara, Ruvuma, Pwani na wajumbe wa Bodi ya Korosho Tanzania (CBT). Wakuu wa Wilaya, baadhi ya Wenyeviti wa Halmashauri na wataalamu kutoka kituo cha utafiti cha Naliendele walishiriki uzinduzi huo.

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU

0 comments:

Mapato ya Korosho Mikoa Minne Yafikia Trilioni Moja


MAPATO kutokana na mauzo ya korosho katika msimu wa 2017/2018 katika mikoa minne ya Lindi, Mtwara, Pwani na Ruvuma yamepanda na kufikia sh. trilioni 1.08 ikilinganishwa na misimu miwili iliyopita.

Kaimu Mkurugenzi wa Bodi ya Korosho Tanzania (CBT), Bw. Hassan Jarufu alitoa taarifa hiyo Jumapili, Desemba 31, 2017 wakati akitoa ufafanuzi juu ya uzalishaji na mauzo ya zao la korosho nchini hadi kufikia mwisho wa mwaka 2017.

“Ukiangalia msimu wa mwaka 2015/2016, utaona kuwa korosho zilizozalishwa zilikuwa kidogo zaidi. Msimu huo ziliuzwa kilo 155,244,645 zikiwa na thamani ya sh. 388,474,530,906.00 ikilinganisha na msimu wa 2016/2017 ambapo jumla ya kilo 265,237,845.00 ziliuzwa zikiwa na thamani ya sh. 871,462,989,284.00,” alisema.

Alisema katika minada 10 ya msimu wa 2017/2018, mauzo ya korosho yamefikia kilo 285,828,205 zenye thamani ya sh. 1,082,200,383,581.00. “Mnada wa 10 ulikuwa tarehe 21 Desemba, 2017 na minada bado inaendelea kwa msimu wa 2017/2018,” alisema.

Akitoa ufafanuzi wa mauzo hayo kwa kila mikoa hadi kufikia mnada wa 10, Bw. Jarufu alisema Mkoa wa Mtwara umeongoza kwa kuuza tani 178,165.741 zenye thamani ya sh. 701,674,466,366.00 ukifuatiwa na mkoa wa Lindi ambao umeuza tani 68,687.504 zenye thamani ya sh. 247,163,294,296.00.

“Mkoa wa Ruvuma umeuza tani 19,545.613 zenye thamani ya sh. 76,173,400,063.00 na mkoa wa Pwani umeuza tani 19,429.347 zenye thamani ya sh. 57,189,224,856.00 na kufanya mapato yote kwa mwaka huu kufikia sh. trilioni 1.082,” alisema.

Bw. Jarufu alitoa ufafanuzi huo mara baada ya Waziri Mkuu Kassim Majaliwa kuzindua kampeni ya kitaifa ya upandaji mikorosho bora na mipya milioni 10 kwa msimu wa 2017/2018 mjini Ruangwa, mkoani Lindi. Kaulimbiu ya kampeni hiyo ni: “Korosho ni dhahabu ya kijani, tuitunze, itutunze”.

Bw. Jarufu alimweleza Waziri Mkuu kwamba Bodi ya Korosho Tanzania kwa kushirikiana na Taasisi ya Utafiti wa Kilimo Naliendele, Sekretarieti za Mikoa na Halmashauri za wilaya, imeendelea kutekeleza mpango wa miaka mitatu wa kupanda mikorosho 10,000,000 kila mwaka.

“Katika mpango huu, wastani wa mikorosho 5,000 inatarajiwa kupandwa katika kila kijiji au mikorosho 30 kwa kaya kwa mwaka, sawa na ekari 330,000 kwa mwaka kwa nchi mzima. Lengo la mpango huu ni kuongeza kiasi cha korosho kinachozalishwa nchini kwa kuongeza wigo wa halmashauri zinazozalisha korosho na kupanda miche inayotokana na mbegu bora zenye uzalishaji mkubwa na zenye ukinzani dhidi ya magonjwa na wadudu,” alisema.

Alisema katika msimu wa 2017/2018, Bodi ya korosho inaratibu uzalishaji wa jumla ya miche 14,001,820 ambayo imetokana na tani 100 (kilo100, 000) zilizozalishwa na Taasisi ya Utafiti wa Kilimo Naliendele.

“Mchanganuo wake ni kama ifuatavyo: kilo 31,170 za mbegu zitapandwa shambani moja kwa moja ambazo zitatoa jumla ya miche 2,181,900; kilo 68,830 zitazalisha jumla ya miche 11,819,920 kati ya miche hiyo isiyobebeshwa ni 9,636,200 na miche itakayobebeshwa ni 2,183,720.

“Ni matumaini yetu kuwa ifikapo mwishoni mwa mwezi Februari 2018, miche yote itakuwa tayari imezalishwa, kugawanywa na kupandwa katika mashamba ya wakulima,” aliongeza.

Mkurugenzi huyo alisema, katika msimu huu eneo la utekelezaji wa mradi limeongezeka kutoka Halmashauri 51 za msimu uliopita 2016/2017 hadi kufikia Halmashauri 90 nchi nzima  ikiwemo mikoa mipya iliyothibitishwa kustawi zao la korosho hapa nchini.

Sherehe hizo zilihudhuriwa na wakuu wa mikoa ya Lindi, Mtwara, Ruvuma, Pwani na wajumbe wa Bodi ya Korosho Tanzania (CBT). Wakuu wa Wilaya, baadhi ya Wenyeviti wa Halmashauri na wataalamu kutoka kituo cha utafiti cha Naliendele walishiriki uzinduzi huo.

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,

0 comments:

Waziri Mkuu Atoa Kadi Za CHF Kwa Wazee 4,000


WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amewataka wakazi wa wilaya ya Ruangwa wajiunge na Mfuko wa Afya ya Jamii (CHF) ili waweze kumudu gharama za matibabu bila kulazimika kuwa fedha taslimu.

Ametoa wito huo mwishoni mwa wiki wakati akizungumza na mamia ya wakazi wa mji wa Ruangwa na vijiji vya jirani katika mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye viwanja vya CWT, mjini Ruangwa, mkoani Lindi.

“Leo hii nimetoa kadi za CHF kwa wazee 4,000 wa wilaya hii. Ninaishukuru Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa kwa kutenga fedha na kuwalipia wazee hawa ili wanufaike na bima hii ya afya kama ambavyo imeelekezwa kwenye Ilani ya Chama cha Mapinduzi.”

“Ninatoa wito kwa wananchi wengine walipie sh. 15,000 kwa mwaka ili wapatiwe kadi kwa ajili ya watu sita wa familia zao; yaani mhusika, mwenza wake na watoto wanne. Bima hii inasaidia kwa vile unapata matibabu hata kama huna fedha taslimu,” alisema.

Waziri Mkuu alikabidhi kadi kwa Mzee Issa Juma Ngalapa, mkazi wa kata ya Nachingwea pamoja na Mzee Suleiman Stola Lihepa wa kijiji cha Kilimahewa, kata ya Nachingwea kwa niaba ya wazee wote waliotakiwa kupatiwa kadi hizo.

Akitoa ufafanuzi juu ya mpango huo, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa Bw. Andrea Chezue alisema mpango wa kutoa kadi za bima ya afya kwa wazee wameuita ‘CHF Endelevu’ kwa sababu walifanya tathmini na kubaini kuwa matibabu yao yana gharama, na yasipolipiwa, dawa zitaisha au wazee hao hawataweza kupatiwa huduma.

“Katika Halmashauri tulifanya utambuzi wa wazee wa kuanzia miaka 60 na kuendelea kwenye vijiji vyote na kubaini kuwa kuna wazee 4,000. Tukaamua Halmashauri iwalipie sh. 15,000 kwa kila wazee sita kama ilivyo katika kaya ili tuweze kuchangia gharama za matibabu yao,” alisema.

“Mzee akipatiwa kadi hii, inakuwa ni ya kudumu, anaitumia miaka yote. Si ya kulipia kila mwaka kama zilivyo zile nyingine. Hadi sasa tumeshatoa kadi kwa wazee 2,700 na tunaendelea kutengeza kadi hadi tukamilishe zote. Tumepanga kuwa kila mwaka, tutafanya utambuzi wa wazee katika vijiji vyote ili wale wanaofikisha umri huo, nao pia waingizwe kwenye mpango huu,” alisema.

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,

0 comments:

Polepole: Lema 2020 utalisikia hewani tu jimbo la Arusha Mjini


Katibu wa Itikadi na Uenezi  wa  Chama Cha Mapinduzi CCM, Humphrey Polepole amemtahadharisha Mbunge wa Arusha Mjini Godbless Lema kwakumwambia kuwa  kipindi hiki ni cha mwisho kuongoza Jimbo hilo la Arusha Mjini.

Hayo yamekuja mara baada ya Mbunge huyo kupitia kurasa zake za twitter kujibizana huku Lema akionyesha kumhoji Polepole kama familia yake huwa inamuelewa kweli anachokizungumza.

“Term ya mwisho Arusha, tunataka Mbunge wa Masuala na si wa Matukio, hata mkichezesha draft ili uende Hai, haitawezekana maana hata “fly to…” maji yako shingoni, na ukiamua kurudia kazi yako ya zamani. anko Siro is very serious,”ameandika Polepole

0 comments:

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumanne ya January 2



0 comments: