NA IS-HAKA OMAR, ZANZIBAR.
MJUMBE wa Kamati kuu ya CCM, Balozi Seif
Ali Idd ameongoza mamia ya wanachama wa Chama na Wananchi kwa ujumla
katika mazishi ya aliyekuwa Katibu wa CCM Wilaya ya Kusini Unguja
Marehemu Hamdani Haji Machano aliyefariki ghafla jana kwa maradhi ya
baridi.
Maziko hayo yamefanyika katika kijiji
cha Donge Shehia ya Mtambile Mkoa wa Kaskazini Unguja, na kuudhuriwa na
wananchi pamoja na baadhi ya wajumbe wa kamati kuu, Halmashauri kuu za
CCM, Wenyeviti , Makatibu wa Mikoa na Wilaya, Wakuu wa Mikoa na Wilaya
za Zanzibar pamoja na Wajumbe wa NEC.
Akizungumza mara baada ya maziko hayo,
Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Dkt.Abdalla Juma Saadalla “Mabodi ”
alisema Chama hicho kimepokea kwa mshituko na masikitiko makubwa
taarifa ya kifo cha Mtendaji huyo na kuwaomba wanafamilia, ndugu na
jamaa kuwa na subira katika kipindi hiki cha msiba.
Ameeleza kwamba marehemu Hamdani alikuwa
ni Kiongozi mwadilifu na mchapakazi na aliyekuwa akijitolea kufanya
kazi kwa bidii huku akisimamia kwa dhati maslahi ya Chama hicho.
Dkt.Mabodi alifafanua kwamba kutokana na
mchango mkubwa uliotolewa na marehemu huyo wakati wa Utumishi wake, CCM
itaendelea kuenzi juhudi hizo kwa kusimamia mamlaka za kiutendaji ndani
ya chama na serikali ili ziendelee kutenda haki kwa wananchi wote.
“Tumepokea kwa mshituko mkubwa kifo cha
Mtendaji mwenzetu na hili ni pengo kubwa linalotakiwa kuzibwa na umoja
wetu katika na kukitumikia chama chetu kwa uzalendo ili kishinde kila
uchaguzi na kuendelea kuongoza dola kusimamia yote mazuri yaliyoachwa na
Marehemu Hamdani.
Pia nakumbuka hivi juzi tu katika ziara
zangu tulikuwa pamoka katika Mkoa wake wa kazi tukishauriana mambo mengi
ya Kiutendaji na kisiasa, naomba Mwenyezi Mungu amjaalie mapumziko mema
na yenye kheri na yeye Amin.”, alieleza Dkt.Shein.
Kwa upande wake Kaimu Katibu Mkuu wa
UVCCM Taifa, Shaka Hamdu Shaka aliweka bayana kwamba Marehemu Hamdani
alisema kwamba ni kada wa kweli yaliyepigana kuona CCM na Jumuiya zake
zinapiga hatua kubwa kimaendeleo.
Naye Mkaazi wa Shehi ya Chanjaani,
Masoud Haji Choum alisema mbali na Marehemu huyo kuwa na ushirikiano
mzuri na viongozi wa chama na serikali pia alikuwa ni mtu aliyekuwa
akipenda kujumuika na jamii katika masuala mbali mbali ya kimaendeleo,
kijamii na kiuchumi.
Akithibitisha mchango wake Marehemu huyo
katika harakati za kisiasa ndani na nje ya Naibu Katibu Mkuu Mstaafu,
Vuai Ali Vuai Alieleza kwamba Hamdani alikuwa ni mtu makini na mkweli
katika utumishi wake na aliyetamani mabadiliko ya kimaendeleo katika
sehemu yake ya kazi na chama kwa ujumla.
Mara baada ya maziko hayo palisomwa wasifu wa marehemu Hamdani kuwa alizaliwa mwaka 1963, huko Donge.
Amewahi kushika nafasi mbali mbali za
uongozi na utendaji ndani ya chama na jumuiya zake baada ya kujiunga na
CCM mwaka 1987 ambapo mwaka 1988 alikuwa katibu wa UVCCM Tawi la Donge
Mtambile mwaka, Katibu wa UVCCM Wilaya ya Kusini hadi kufikiwa na mauti
alikuwa ni Katibu wa CCM Wilaya ya Kusini Unguja.
Mwenyezi mungu amlaze mahali pema peponi Amin.






















Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki
Mhe. Dkt. Susan Kolimba amekutana na kufanya mazunguzo na Mabalozi
Wateule wanaoenda kuiwakilisha Tanzania maeneo mbalimbali
Duniani.Mazungumzo hayo yaliyofanyika ofisini kwake Makao Makuu ya Nchi
mjini Dodoma, yalijikita katika kujadili namna bora ya kuiwakilisha
Tanzania ughaibuni kwa kuzingatia sera ya nchi ya mambo ya nje, kwa
lengo la kuboresha mahusiano ya Kidiplomasia baina ya Tanzania na nchi
hizo, na kwa kuzingatia maslahi mapana ya kiuchumi ya nchi yetu ikiwemo
kutangaza shughuli za utalii zinazopatikana nchini. 



Katibu Mkuu Wizara ya Maji na Umwagiliaji Prof. Kitila Mkumbo
amesaini kandarasi zenye thamani ya dola za Marekani Milioni 268.35
ambazo ni zaidi ya Shilingi bilioni 600 za Tanzania mjini Tabora kwa
mkopo wa benki ya Exim ya nchini India kwa kushirikiana na Serikali ya
Tanzani kwa ajili ya ujenzi wa mradi wa maji kutoa Ziwa Victoria na
kupeleka katika Manispaa ya Tabora na Halmashauri za Igunga, Uyui,
Shinyanga Vijijini na Nzega. 


Follow Us
Were this world an endless plain, and by sailing eastward we could for ever reach new distances